IQNA

Ban Ki-moon ana wasi wasi kuhusu ujenzi wa vitongoji vya Wazayuni

22:26 - December 13, 2011
Habari ID: 2238269
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban ki-Moon ameelezea ‘wasi wasi mkubwa’ kuhusu ripoti kuwa utawala haramu wa Israel umeidhinisha ujenzi wa vitongoji vya walowezi wa Kizayuni katika ardhi za Palestina unaozikalia kwa mabavu.
Katika taarifa kwa vyombo vya habari, Ban Ki-moon ameutaka utawala haramu wa Israel kusitisha mara moja ujenzi wa vitongoji hivyo katika mji wa Beit Lahm. Amesema ujenzi wa vitongoji hivyo unakiuka sheria za kimataifa.
Nayo Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu OIC ilitoa taarifa hapo siku ya Jumamosi ikilaani vikali uamuzi wa utawala haramu wa Israel wa kujenga vitongoji vipya vya walowezi wa Kiyahudi katika eneo la Ras al-Amud katika kata ya kati huko Quds Tukufu.
Ekmeleddin Ihsanoglu, Katibu Mkuu wa OIC amesema kwamba kuendelea miradi ya ujenzi wa vitongoji vipya vya walowezi wa Kiyahudi katika ardhi za Wapalestina ni jambo linalokwenda kinyume na sheria za kimataifa pamoja na maazimio ya Umoja wa Mataifa.

914926
captcha