IQNA

Maombolezo ya siku 10 za mwisho za mwezi wa Safar kufanyika Hamburg

11:13 - January 09, 2012
Habari ID: 2253782
Kituo cha Kiislamu cha Hamburg kimepanga kufanya maombolezo ya siku kumi za mwisho za mwezi wa Safar katika kituo hicho kuanzia tarehe 13 hadi 23 Januari.
Katika kipindi hicho cha siku 10 ratiba mbalimbali za maombolezo ya Arbaini ya Imam Hussein (as), makumbusho ya kifo cha Mtume (saw) na kuuawa shahidi Maimamu Hassan Mutaba na Imam Ali bin Musa ar-Ridha (as) zitatekelezwa.
Kwa mnasaba huohuo, maombolezo mengine kama hayo ya siku 10 yamepangwa kufanyika katika Kituo cha Kiislamu cha London kuanzia tarehe 14 Januari ambayo inasadifiana na Arbaini ya Imam Hussein (as).
Wanazuoni na wanafikra wa Kiislamu wamepangiwa kuzungumza katika maombolezo hayo kuhusiana na pande mbalimbali za maisha na kujitolea kwa watukufu hao katika kulinda dini tukufu ya Kiislamu. 931628
captcha