IQNA

Kushiriki kwa wingi Wairani katika uchaguzi ni pigo kwa maadui

18:00 - March 03, 2012
Habari ID: 2284633
Khatibu wa Sala ya Ijumaa mjini Tehran amesema kuwa, ushiriki mkubwa wa wananchi wa Iran katika duru ya tisa ya uchaguzi wa Bunge utasambarisha njama za maadui kama ilivyokuwa huko nyuma.
Sheikh Kazem Sidiqi amesema hayo mbele ya hadhara kubwa ya waumini waliohudhuria ibada ya Sala ya Ijumaa na kubainisha kwamba, ushiriki mkubwa wa wananchi katika uchaguzi wa Bunge uliofanyika leo ni pigo kubwa kwa maadui wa taifa hili. Khatibu wa Sala ya Ijumaa ameashiria pia njama za maadui dhidi ya Mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu unaotawala hapa nchini na kusema kwamba, kama ilivyokuwa huko nyuma wananchi wa Iran wataleta hamasa nyingine kwa kushiriki kwa wingi katika uchaguzi na kumkatisha tamaa adui. Amesema, propaganda kubwa za maadui ni ishara ya woga na wasi wasi mkubwa walionao maadui kwa taathitra ya Mapinduzi ya Kiislamu katika eneo hili. Sheikh Kazem Sidiqi ameashiria kitendo cha kishenzi cha hivi karibvuni cha wanajeshi wa Marekani cha kuivunjia heshima Qur'ani tukufu kwa kuichoma moto huko Afghanistan na kusema, kitendo hicho cha wananjeshi wa Marekani ni kuwatusi na kuwanjia heshima wanadamu na vitabu vingine vya mbinguni.
963716
captcha