Wachezaji Hatem Ben Arfa, Papiss Cisse na Demba Ba ni miongoni mwa nyota wa timu ya Newcastle United msimu huu na kocha wao Alan Pardew ana matumaini kwamba wataisaidia timu hiyo kufanya vyema zaidi.
Kocha Perdew anaamini kuwa itikadi za kidini za wachezaji hao watatu Waislamu zimekuwa na mchango muhimu katika mafanikio ya klabu hiyo katika msimu huu wa ligi ya Premier.
Kocha wa Newcastle ameliambia gazeti la The Mail kwamba amezungumza na mkurugenzi wa klabu hiyo kuhusu suala la ujenzi wa eneo la ibada ya Swala kwa ajili ya wachezaji hao Waislamu kwani viongozi wa klabu wanalazimika kulinda itikadi za kidini za wachezaji wake.
Alan Pardew ameongeza kuwa wachezaji wanapaswa kuheshimiwa na kwamba wachezaji wa ligi kuu ya Uingereza wanafuata dini mbalimbali na kuna udharura wa kujali hali zao. 1001869