IQNA

Kisomo cha makarii wa Iran pembeni ya al Kaaba Tukufu

13:07 - June 28, 2012
Habari ID: 2356304
Makarii na wasomaji wa Qur'ani wa Iran wamesoma aya za kitabu hicho kandokando ya nyumba tukufu ya Mwenyezi Mungu al Kaaba.
Mwandishi wa IQNA mjini Makka amesema, katika majlisi hiyo ya kiraa ya Qur'ani iliyoundwa na msafara wa kwanza wa wasomaji Qur'ani kutoka Iran waliokwenda kutekeleza ibada ya umra, walimu, makarii na mahufadh wa Qur'ani Tukufu, wasimamizi wa vituo vya Qur'ani nas maqarii kadhaa mashuhuri wa Iran waliwafurahisha watu waliokwenda kutufu nyumba ya Mwenyezi Mungu kwa kiraa ya aya za Qur'ani ambayo imewavutia watu wengi.
Baada ya hapo makarii wa Iran waligawana juzuu 30 za Qur'ani Tukufu na kuhitimisha Qur'ani nzima.
Katika majlisi hiyo makarii wa Kiirani pia walisoma dua, ziara na kufanya ibada ya twawafu. 1039625

captcha