IQNA

Uingereza yalaaniwa kwa kuunga mkono jinai za tawala za Bahrain na Saudia

16:16 - July 15, 2012
Habari ID: 2368759
Waandamanaji waliokuwa na hasira wameandamana nje ya balozi za Bahrain na Saudi Arabia mjini London kulaani jinai za tawala hizo mbili za kifalme dhidi ya wananchi wanaoandamana kutaka demokrasia.
Aidha waandamanaji wamelaani serikali ya Uingereza kwa kuendelea kuunga mkono tawala hizo mbili katili.
Maandamano hayo ya Jumamosi yameandaliwa na Harakati ya Uhuru ya Bahrain na wanaharakati wanaopinga vita kutoka muungano wa Stop the War.
Maandamano hayo ya London yamefanyika huku utawala wa Saudi Arabia ukiendelea kuwakandamiza waandamanaji mashariki mwa nchi hiyo. Katika kipindi cha wiki moja iliyopita, Wasaudi wanne wameuawa shahidi kufuatia hujuma ya vikosi vya ufalme wa Aal Saud dhidi ya wananchi wanaoandamana kwa amani.
Aidha utawala wa kifalme wa Aal Khalifa nchini Bahrain unaendelea kuwakandamiza waandamanaji na sasa maandamano ya wapinzani yamepigwa marufuku. Pamoja na ukatili huo, Uingereza inayodai kutetea haki za binadamu inaendelea kuziuzia tawala hizo silaha za kukabiliana na waandamanaji.
1053116
captcha