IQNA

Rais Ahmadinejad atoa salamu za Ramadhani kwa Waislamu wote duniani

16:38 - July 21, 2012
Habari ID: 2373795
Rais Mahmoud Ahmadinejad wa Jamhuri ya Kiislamu za Iran ametoa salamu za kheri na fanaka kwa viongozi wa mataifa ya Waislamu kote duniani kwa munasaba wa kuwadia Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
Katika ujumbe wake, Rais Ahmadinejad ametoa wito wa umoja katika Ulimwengu wa Kiislamu.
Katika barua tafauti alizowaandikia viongozi wa nchi za Waislamu pamoja na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu OIC, Rais Ahmadinejad ameelezea matumaini kuwa katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani, ulimwengu utashuhudia ‘urafiki na udugu miongoni mwa mataifa ya dunia hasa mataifa ya Waislamu.’ Aidha amesema ana matumaini kuwa dhulma na ubaguzi utafika ukingoni na dunia kushuhudia amani na usalama wa kudumu.
Rais Ahmadinejad amewatakia furaha na ufanisi Waislamu kote duniani.
1058446
captcha