IQNA

Misaada yakusanywa katika maonyesho ya Qur'ani ya Tehran kwa ajili ya Waislamu wa Myanmar

17:26 - July 23, 2012
Habari ID: 2375757
Kibanda maalumu cha 'Mataifa na Umoja' kimeanzishwa katika maonyesho ya 20 kimataifa ya Qur'ani mjini Tehran kwa lengo la kukusanya misaada ya kibinadamu ya wageni wanaotembelea maonyesho hayo kwa ajili ya kuwasaidia Waislamu wa Myanmar wanaouawa kinyama na utawala dhalimu wa nchi hiyo.
Kitengo hicho pia kinaonyesha picha mbalimbali za video za mauaji ya kinyama na mateso wanayofanyiwa Waislamu hao wasio na wa kuwatetea ili kuwafahamisha walimwengu machungu wanayoyapitia.
Misaada hiyo inatazamiwa kutumwa kwa Waislamu hao katika siku za Leilatul Qadr. Mwaka uliopita kitengo hicho pia kilikusanya misaada kama hiyo kwa ajili ya Waislamu waliokumbwa na njaa wa Somalia na pia waliokumbwa na janga la mafuriko nchini Pakistan.
Maonyesho ya kimataifa ya Qur'ani yanayofanyika katika Muswala wa Imam Khomeini chini ya anwani ya 'Qur'ani, Utamaduni wa Mwamko' yalianza tarehe 15 Julai na yatazamiwa kuendela kwa kipindi cha karibu mwezi mmoja. 1060374
captcha