IQNA

Jumuiya ya Ulinganiaji wa Kiislamu Libya yatoa wito wa kuwatetea Waislamu wa Myanmar

18:01 - July 31, 2012
Habari ID: 2382311
Jumuiya ya Ulinganiaji wa Kiislamu ya Libya imetoa taarifa ikilaani mauaji yanayoendelea kufanywa dhidi ya jamii ya Waislamu huko Myanmar na imezitaka jumuiya zote za wanasheria duniani kuonyesha mshikamano na Waislamu hao wanaodhulumiwa.
Gazeti la Libya al Youm limeripoti kuwa Jumuiya ya Ulinganiaji wa Kiislamu imesema katika taarifa hiyo kwamba vitendo vya ubaguzi wa kizazi, mauaji ya halaiki na kuwalazimisha Waislamu kuwa wakimbizi huko Myanmar vinapaswa kulaaniwa vikali. Imesema inasikitisha kuwa jamii ya kimataifa imenyamazia kimya jinai na mauaji hayo.
Taarifa hiyo imehoji: "Vipi maelfu ya Waislamu wa Myanmar wanashambuliwa, kuuawa na kulazimishwa kukimbia makazi yao na kundi moja la watenda jinai huku jamii ya kimataifa ikiendelea kunyamaza kimya?
Jumuiya ya Ulinganiaji wa Kiislamu ya Libya imeyataka mataifa, serikali na jumuiya za kisheria kote duniani kupaza sauti ya kupinga jinai zinazofanyika nchini Myanmar dhidi ya Waislamu wa nchi hiyo na kutumia mbinu mbalimbali kulaani jinai hizo ikiwa ni pamoja na mbinu ya vikwazo vya kiuchumi. 1067246

captcha