IQNA

Maonyesho ya kazi za wasanii wa Kiirani katika medani ya Qur'ani Uturuki

20:03 - August 01, 2012
Habari ID: 2383388
Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inaonyesha athari na kazi za wasanii wa Kiirani katika nyanja za Qur'ani kwenye mji wa Erzurum huko mashariki mwa Uturuki.
Televisheni ya Press imeripoti kuwa kitengo cha utamaduni cha Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika mji wa Erzurum kimetangaza kuwa maonyesho hayo ya kazi za kisanii zinazohusiana na Qur'ani Tukufu yanafanyika kwa mnasaba wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Karibu kazi 100 za kisanii zinazohusiana na Qur'ani zinaonyeshwa katika maonyesho hayo.
Ofisi ya kituo cha utamaduni cha Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika mji wa Erzurum pia imeandaa vikao vya kiraa ya Qur'ani Tukufu ambavyo vinahudhuriwa na makarii wa Kiirani na Kituruki. 1068272
captcha