Maduka ya kuuza vitabu nchini Uingereza yanaripoti kuwa, uuzaji vitabu vya Kiislamu umeongezeka kwa asilimia 30 nchini humo baada ya kutolewa filamu ya Innocence of Muslims inayomtusi Mtume Muhammad (saw).
Ripoti zinasema kuwa baada ya kutazama filamu hiyo ya Kimarekani Waingereza wasio Waislamu wamekuwa na hamu kubwa ya kuujua Uislamu na wamekuwa wakinunua kwa wingi vitabu vinavyohusiana na dini hiyo ya Mwenyezi Mungu.
Vilevile tarjumi ya lugha ya Kiingereza ya Qur’ani Tukufu ni miongoni mwa vitabu vinavyouzwa kwa wingi nchini humo. 1104763