IQNA

Kongamano la nane la kimataifa la Qur'ani kufanyika Uingereza

17:09 - March 30, 2013
Habari ID: 2513998
Kongamano la nane la kimataifa la Qur'ani Tukufu litafanyika mjini London, Uingereza chini ya usimamizi wa Kitivo cha Utafiti wa Masuala ya Mashariki na Afrika (SOAS).
Kongamano hilo litaongozwa na Profesa Muhammad Abdulhalim ambaye ni mtarjumi wa Qur'ani Tukufu na Helen Blatherwick, mhadhiri wa fasihi ya lugha ya Kiarabu katika Chuo Kikuu cha London.
Kongamano hilo limepangwa kufanyika tarehe 20 hadi 22 Novemba na litachunguza utafiti wa matini ya Qur'ani, tafsiri na tarjumi za kitabu hicho cha Mwenyezi Mungu.
Lengo la kongamano hilo ni kuchunguza masuala mbalimbali yanayohusu matini, tafsiri na tarjumi ya Qur'ani.
Makala zitakazochaguliwa katika kongamano hilo zitachapishwa katika jarida la utafiti wa Qur'ani la Chuo Kikuu cha London. 1206149

captcha