Vijana hao wamelaani vikali kitendo cha maafisa wa jela ya al Hair cha kuvunjia heshima Qur'ani Tukufu. Waandamanaji hao wametoa wito wa kufikishwa mahakamani maafisa wa jela hiyo waliovunjia heshima Qur'ani, kufutwa kazi Waziri wa Mambo ya Ndani wa Saudia Muhammad bin Nayif na kuachiwa huru wafungwa wote wanaoshikiliwa katika jela hiyo.
Wafungwa wanaoshikiliwa katika jela hiyo wamewaambia jamaa zao kwamba maafisa wa jela wamerusha chini na kuzipiga teke nakala za Qur'ani Tukufu kwa shabaha ya kuchochea hisia za wafungwa hao.
Askari usalama wa serikali ya Saudia walipelekwa katika jela ya Hair baada ya wafungwa wa jela hiyo kupinga kitendo cha kuvunjiwa Qur'ani Tukufu. 1213793