Mkuu wa Kituo cha Masuala ya Qur'ani Tukufu cha Taasisi ya Wakfu na Masuala la Kheri cha Iran amesema kuwa, mahafali 420 ya kuwa na mapenzi na ukuruba na Qur'ani Tukufu yatafanyika katika pembe mbalimbali za Iran yakiwashirikisha maqarii 8 bingwa wa Misri na yataendelea katika siku zote za mwezi huu mtukufu wa Ramadhani.