IQNA

Maonyesho ya nakala za kale za Qur'ani kufanyika Najaf

20:49 - October 28, 2013
Habari ID: 2609671
Maonyesho ya pili ya nakala za Qur'ani Tukufu zilizoandikwa kwa hati za mkono imepangwa kufanyika tarehe 30 mwezi huu wa Oktoba katika mji mtakatifu wa Najaf huko Iraq.
Maonyesho hayo yanasimamiwa na kamati ya maandalizi ya Tamasha la Kimataifa la Ghadir na yatafanyika katika Haram ya Imam Ali bin Abi Twalib (as) mjini Najaf.
Katika maonyesho hayo ya siku tatu kutaoneshwa nakala za Qur'ani Tukufu zilizoandikwa kwa hati za mkono katika karne ya kwanza hadi ya nne Hijria.
Msimamizi wa maonyesho hayo ya Qur'ani amesema maandalizi yanaendelea ndani ya Haramu ya Imam Ali (as) na kwamba nakala za Qur'ani Tukufu zilizoandikwa kwa hati za mkono na zilizopambwa kwa maji ya dhahabu zitaonyeshwa katika shughuli hiyo.
Hashim Muhammad Murtadha amesema msahafu unaonasibishwa kwa Imam Ali bin Abi Twalib (as) ambao uliandikwa mwaka 40 Hijria pia utaonyeshwa katika maonyesho hayo ya Qur'ani. 1308844

captcha