Duka la kuuza vitabu ya La Procure mjini Paris imeripoti kuwa, idadi ya nakala za Qur'ani zilizouzwa katika siku za baada ya mashambulzi hayo imeongeza ghafla.
Afisa wa masuala ya kidini wa duka hilo la kuuza vitabu amesema hii ni mara ya kwanza kushuhudiwa ongezeko kubwa kiasi hiki cha ununuzi wa idadi kubwa zaidi ya nakala a Qur'ani.
Amesema wakati wa kurushwa hewani filamu ya matukio ya kweli ya Watawa wa Tibhirine (Monks of Tibhirine) inayohusu watawa saba wa Kifaransa waliouawa na makundi ya kigaidi katika mkoa wa Medea nchini Algeria mwaka 1996, idadi ya ununuzi wa vitabu vinavyohusu Uislamu na uhusiano wa Waislamu na Wakristo iliongezeka lakini hii ni mara ya kwanza kuongezeka ununuzi wa nakala za Qur'ani. AIR