IQNA

Waislamu Ethiopia wafungwa jela kwa tuhuma za 'ugaidi'

19:24 - August 05, 2015
Habari ID: 3339480
Waislamu nchini Ethiopia wamelaani uamuzi wa mahakama moja ya nchi hiyo ya kuwafunga jela miaka 22 wanaharakati 18 wa Kiislamu kwa tuhuma eti za ugaidi.

Taarifa iliyotolewa na Muungano wa Waislamu nchini humo imesema kesi za wanaharakati hao zimetiwa chumvi kutokana na misimamo yao dhidi ya dhulma za serikali kwa WaislamuWanaharakati  hao 18 walishtakiwa mwezi uliopita kwa tuhuma kadhaa likiwemo suala la ugaidi na njama ya kubuni taifa la Kiislamu. Wamekana mashtaka hayo na kulalama kwamba walinyanyaswa wakati walipokuwa kizuizini. Wakati wa ziara ya rais Barack Obama nchini humo, baadhi ya wanaharakati walimueleza kuhusu kesi hiyo ambapo inadaiwa aliitaka serikali ya Addis Ababa iwaachilie huru.

3339148

captcha