IQNA – Makumbusho yaliyojitolea kuhifadhi historia na utamaduni wa Waislamu wa Kitatar yanatarajiwa kuzinduliwa nchini Poland.
Habari ID: 3482612 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/08/11
IQNA – Kupokea vijana Waislamu na kuwapatia programu za kidini na Qur’ani huifanya misikiti nchini Brazil kuimarisha hali yao ya kiroho, huku pia ikilea kizazi kipya kilichounganishwa na Qur’an na Sunna ya Mtume SAW.
Habari ID: 3482606 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/08/09
IQNA – Vyombo vya habari vya Israel vimeonyesha wasiwasi kufuatia ushindi wa daktari Mmisri-Mmarekani, Abdul El-Sayed, katika kura za mchujo za Chama cha Democratic kwa kiti cha Seneti ya Marekani katika jimbo la Michigan, vikilitaja tukio hilo kuwa pigo muhimu kwa makundi yanayounga mkono Israel nchini Marekani.
Habari ID: 3482593 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/08/07
IQNA – Baraza la Jiji la McKinney, jimboni Texas nchini Marekani, limeidhinisha kwa kauli moja mpango wa kujengwa kwa msikiti mpya uliopendekezwa na Jumuiya ya Kiislamu ya McKinney, licha ya wasiwasi uliotolewa na baadhi ya wakazi kuhusu athari zinazoweza kujitokeza kwa jamii inayozunguka eneo hilo. Uamuzi huo wa kura 7-0 ulifuatia kikao kirefu na wakati mwingine chenye mvutano, ambapo takriban wakazi 150 walizungumza, baadhi wakiunga mkono na wengine wakipinga mradi huo.
Habari ID: 3482592 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/08/07
IQNA - Tamasha la Salam 2026 limefanyika nchini Kosovo kwa ushiriki wa familia za Kiislamu, sambamba na uwasilishaji wa programu za kitamaduni na kisanii.
Habari ID: 3482546 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/07/28
IQNA – Taasisi ya British Muslim Trust (BMT) imebainisha kuwa, kwa wastani, msikiti mmoja hushambuliwa kila baada ya siku tano nchini Uingereza.
Habari ID: 3482532 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/07/25
IQNA – Mfanyakazi mmoja Mwislamu wa vibanda vya biashara amechomwa kisu zaidi ya mara 15 ndani ya kituo cha ununuzi (mall) huko Utah, Marekani, na mtu ambaye baadaye alikiri kwa polisi kuwa alikusudia kumuua “kwa sababu ya dini yake.”
Habari ID: 3482498 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/07/17
IQNA – Mamlaka za Uingereza zimemfungulia mashtaka kijana mmoja kufuatia uchunguzi wa njama zilizodaiwa kuwa zililenga kushambulia misikiti katika jiji la London.
Habari ID: 3482495 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/07/17
IQNA – Kituo cha Kiislamu cha Vienna, jijini Vienna nchini Austria, kimekaribisha makundi ya wanafunzi kutoka shule mbalimbali nchini humo siku kadhaa kabla ya kuanza kwa likizo ya masomo.
Habari ID: 3482479 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/07/13
iQNA – Kundi la wanawake Waislamu katika eneo la kaskazini-mashariki mwa Kenya limefanikiwa kugeuza ari ya kujitolea kuwa mradi wa maendeleo unaochanganya uwezeshaji wa wanawake kiuchumi, huduma kwa Qur’an Tukufu, na kuimarisha mshikamano wa kijamii.
Habari ID: 3482426 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/07/01
IQNA – Toleo la saba la Siku ya Wanawake Waislamu limefanyika jijini Bangkok kwa ushiriki wa makumi ya wanawake Waislamu kutoka misikiti na jamii mbalimbali za Kiislamu nchini Thailand.
Habari ID: 3482377 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/19
IQNA – Misikiti kote nchini Uingereza imehimizwa kufanya mazoezi ya taratibu za kujifungia (lockdown) na kuimarisha hatua za usalama kufuatia mwongozo mpya wa kitaifa, huku viongozi wa jamii wakionya juu ya kuongezeka kwa matukio ya chuki dhidi ya Uislamu na shughuli za makundi ya mrengo mkali wa kulia.
Habari ID: 3482375 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/19
IQNA – Sauti za dua, takbira na furaha zilitawala anga ya Dearborn Heights, Michigan nchini Marekani huku mamia ya watu wakikusanyika kukata utepe wa ufunguzi wa Msikiti wa Imam Al‑Hasanain na makao makuu mapya ya Taasisi ya Kiislamu ya Amerika (IIOA).
Habari ID: 3482357 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/13
IQNA – Mamlaka katika mji mkuu wa jimbo la Arunachal Pradesh nchini India zimezifunga misikiti yote 15 iliyoko katika mji huo mkuu, hatua iliyozua ukosoaji na malalamiko kutoka kwa makundi ya Kiislamu.
Habari ID: 3482355 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/13
IQNA – Suleiman Ashirlayev, msanii wa khatt kutoka Jamhuri ya Dagestan katika Shirikisho la Urusi, ameandika Qur’ani Tukufu nzima kwa maandishi ya Thuluth katika tajiriba aliyoiita ya kiroho.
Habari ID: 3482344 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/09
Waislamu wa China
IQNA – Kwa kutegemea mradi wa kielimu ulioendelea kwa zaidi ya miaka ishirini, Msikiti Mkuu au Msikiti wa Jamia wa Taipei katika eneo la China la Taiwan umejidhihirisha kama mfano wenye mafanikio katika kulea na kuelimisha vizazi vijavyo vya Waislamu.
Habari ID: 3482333 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/07
IQNA – Miaka mitano baada ya washiriki wanne wa familia moja ya Kiislamu kuuawa kwa kugongwa makusudi na gari katika kitendo ambacho jaji amekitaja kuwa ni cha kigaidi, wanajamii katika mji wa London, Ontario nchini Kanada, wamekusanyika kuwakumbuka wahanga hao na kusisitiza upya ahadi yao ya kupambana na chuki dhidi ya Uislamu (Islamophobia).
Habari ID: 3482332 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/07
IQNA – Polisi wanawatafuta washukiwa baada ya msikiti mmoja katika mji wa Moncton, ulioko kusini-mashariki mwa jimbo la New Brunswick nchini Kanada, kuharibiwa kwa maandishi ya kuta (graffiti) yenye chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu. Waumini wa msikiti huo wanasema kitendo hicho ni shambulio lililolenga moja kwa moja jamii yao ya Kiislamu.
Habari ID: 3482328 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/06
IQNA – Miaka mitano baada ya mwanaume mmoja kuendesha kwa makusudi gari aina ya pickup na kuigonga familia ya Kiislamu iliyokuwa ikitembea kwa miguu mjini London, katika jimbo la Ontario, Kanada, na kuwaua watu wanne, kundi la kitaifa la utetezi wa haki za Waislamu limesema kuwa serikali ya shirikisho imeshindwa kutekeleza mapendekezo muhimu ya kukabiliana na chuki dhidi ya Uislamu.
Habari ID: 3482323 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/05
IQNA – Kituo cha Kiislamu cha Vila Cahón huko São Paulo, nchini Brazil, kina nafasi kubwa zaidi ya kuwa taasisi ya kidini pekee.
Habari ID: 3482313 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/02