IQNA – Sheikh Chems-Eddine Hafiz, mlezi wa Msikiti Mkuu wa Paris, amesema mwaka 2025 ulikuwa miongoni mwa miaka migumu zaidi kwa Waislamu nchini Ufaransa, ukitawaliwa na matukio ya vurugu yaliyofikia kiwango cha “kuuawa kwa misingi ya dini.”
Habari ID: 3481766 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/04
IQNA – Sheikh Ahmed Ahmed Nuaina, qari mashuhuri kutoka Misri, alisoma Qur’an katika msikiti wa Milwaukee, jimbo la Wisconsin, Marekani, Jumamosi jioni.
Habari ID: 3481762 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/04
IQNA – Wakati wengi walikusanyika na familia zao, milango ya msikiti mmoja mjini Bradford, kaskazini mwa Uingereza, ilifunguliwa kuwapokea wale ambao vinginevyo wangebaki peke yao.
Habari ID: 3481744 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/31
IQNA – Mapinduzi ya kimyakimya ya upishi yanaendelea mjini Seoul, Korea Kusini yakichochewa na mifuko na ladha za kundi linalokua kwa kasi: watalii Waislamu.
Habari ID: 3481732 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/29
IQNA – Kuanzia unyanyasaji wa mtandaoni hadi mashambulizi ya umati na sera za kibaguzi, mwaka 2025 uliweka bayana hali ya kutisha kwa Waislamu walio wachache nchini India.
Habari ID: 3481726 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/28
IQNA- Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, amesema kuwa, Jamhuri ya Iran ya Kiislamu ni mbeba bendera ya kukabiliana mfumo wa kibeberu na mlinganiaji wa kuwepo mfumo wa kiadilifu wa Kiislamu ulimwenguni; suala ambalo kwa mujibu wake, ndilo sababu kuu ya mkanganyiko wa mataifa makubwa.
Habari ID: 3481725 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/28
IQNA – Kituo cha Kiislamu cha Vila Cajon kilichoko Sao Paulo, mji mkuu wa kiuchumi wa Brazil, kimeandaa kozi ya kuhifadhi Qur’ani Tukufu kwa watoto.
Habari ID: 3481721 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/27
IQNA-Baada ya mkasa wa Bondi uliouunganisha taifa katika huzuni, Waislamu wengi wa Australia wanakabiliwa na hali ya kutisha sambamba: kuongezeka kwa matusi na vitisho vinavyowalaumu kimakosa kwa shambulio hilo.
Habari ID: 3481708 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/24
IQNA – Msikiti wa Fakhrul-Muslimin, maarufu kama “Fakhari ya Waislamu”, ulioko nchini Urusi, unavutia idadi kubwa ya wageni kutokana na usanifu wake wa kipekee.
Habari ID: 3481703 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/23
IQNA – Ujumbe wa ngazi ya juu wanazuoni wa Kiislamu kutoka Georgia umezuru Haram ya Imam Ridha (AS) jini Mashhad, Iran, ambapo wamekutana na maafisa wa Astan Quds Razavi (AQR), taasisi inayosimamia haram hiyo tukufu.
Habari ID: 3481664 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/15
IQNA – Kitendo cha kudhalilisha na kuivunjia heshima Qur’ani Tukufu kilichotokea mjini Plano, jimbo la Texas, Marekani, kimezua hasira kubwa miongoni mwa wananchi na mashirika ya haki za binadamu.
Habari ID: 3481659 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/14
IQNA – Katika jiji la Dearborn, Michigan, kuna taasisi ya Kishia iliyodumu kwa miaka mingi, ikifanya kazi kimya kimya bila makuu, lakini ikiwa na athari kubwa katika jamii.
Habari ID: 3481658 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/14
IQNA – Kituo cha Kimataifa cha Uislamu kwa Uvumilivu na Amani nchini Brazil kimeanzisha mpango maalumu wa kielimu wiki hii katika uwanja wa tafsiri ya Qur’ani Tukufu na kusoma Hadith za Mtume (SAW).
Habari ID: 3481618 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/05
IQNA – Seneta mwenye msimamo mkali wa mrengo wa kulia nchini Australia, Pauline Hanson, ameibua hasira kali Jumatatu baada ya kuingia bungeni akiwa amevaa vazi la Waislamu la burka, kama sehemu ya juhudi zake za mara kwa mara za kutaka vazi hilo lipigwe marufuku kwa sababu eti wanaovaa hufunika uso wote hadharani.
Habari ID: 3481565 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/25
IQNA – Mashirika kadhaa ya Kiislamu nchini Ufaransa yamekosoa taasisi ya utafiti wa maoni ya wananchi, IFOP, kwa kile walichokiita upendeleo wa wazi na kuvunja viwango vya maadili ya kitaaluma.
Habari ID: 3481564 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/25
IQNA – Mkutano wa 38 wa Kimataifa wa Waislamu wa Amerika ya Kusini na Karibiani unafanyika nchini Brazil, ukikusanya viongozi wa Kiislamu kujadili mada ya vijana Waislamu katika enzi ya akili mnemba (AI).
Habari ID: 3481553 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/22
IQNA – Kamati ya Masuala ya Katiba ya Ureno imeamua kuwa pendekezo la kuzuia ufadhili wa umma kwa ujenzi wa misikiti halina msingi wa kikatiba.
Habari ID: 3481549 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/21
IQNA – Baada ya tukio la uhalifu wa chuki lililoripotiwa ambapo dada Muislamu alivamiwa na kufuatwa karibu na Chuo Kikuu cha Columbia kwa sababu ya kuvaa niqab, taasisi hiyo imetoa tamko la kulaani shambulio hilo hadharani.
Habari ID: 3481522 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/16
IQNA – Mradi wa kutafsiri Qur'an kwa lugha ya Rohingya umeanzishwa katika mazingira ambapo Waislamu wa Rohingya wamekuwa wakilengwa na dhulma na kufukuzwa kutoka ardhi yao kwa miongo kadhaa. Lengo lake ni kuziba pengo la maarifa ya Kiislamu na kupambana na ukandamizaji wa lugha ya Rohingya.
Habari ID: 3481493 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/09
IQNA-Katika ripoti mpya iliyotolewa na taasisi ya utafiti ya Uswidi, imebainika kuwa idadi kubwa ya wanafunzi Waislamu wamekuwa wakihama shule kutokana na kukumbwa na ubaguzi wa rangi na chuki dhidi ya Uislamu.
Habari ID: 3481482 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/07