IQNA

Kiongozi Muadhamu: Iran na Uturuki zinaweza kuimarisha uhusiano

12:27 - February 01, 2014
Habari ID: 1368993
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Uturuki zina uwezo mkubwa unaoweza kusaidia kuimarishwa zaidi mashirikiano ya pande mbil

Akizungumza na Racep Tayyep Erdogan Waziri Mkuu wa Uturuki aliyeko hapa nchini, Ayatullahil Udhma Ali Khamenei ameongeza kuwa, udugu,upendo na urafiki ulioko kati ya Iran na Uturuki hauna mfano wake  katika karne za hivi karibuni na kusisitiza kwamba uwezo mkubwa uliokuwa nazo pande hizo mbili, unapasa kuandaa mazingira ya kuimarishwa zaidi mashirikiano ya Tehran na Ankara. Ayatullah Khamenei amesisitiza juu ya kutekelezwa makubaliano yaliyotiwa saini kwenye safari ya Waziri Mkuu wa Uturuki mjini Tehran na kuongeza kuwa, iwapo pande mbili zitakuwa jaddi, bila shaka kutashuhudiwa kuimarishwa na kustawishwa zaidi mashirikiano ya pande mbili. Kwenye mazungumzo hayo, naye Waziri Mkuu wa Uturuki amefikisha salamu za rais na wananchi wa Uturuki na kusema kwamba, wananchi wa Uturuki wanaamini kwamba Iran ni makazi yao ya pili. Erdogan  amesema kuwa, mazungumzo aliyoyafanya leo na Rais Hassan Rouhani na viongozi wengine wa ngazi  za juu hapa nchini yamekuwa na  mafanikio na kusisitiza kwamba, Ankara ina matumaini kwamba uhusiano wa pande mbili ambao umekuwa  ukiongezeka siku hadi siku, ni kigezo kwa eneo  la Mashariki ya Kati na ulimwenguni.

http://www.iqna.ir/fa/News/1368331

Kishikizo: ulimwenguni
captcha