
Maonesho haya yanayofanyika katika ukumbi mkubwa wa Jeddah Superdome yamelenga kuwaleta pamoja wadau wa serikali, sekta binafsi na mashirika ya kimataifa ili kujadili mustakabali wa utoaji wa huduma za Hija.
Kwa mujibu wa waandaaji, lengo kuu la mkutano huu ni “kuunganisha juhudi za maandalizi ya msimu ujao wa Hija, kuweka mwelekeo wa huduma za baadaye za Hija, na kuinua kiwango cha huduma kwa mahujaji kwa kuzingatia viwango vya kimataifa vya hali ya juu.”
Zaidi ya mataifa 150 na mashirika mbalimbali ya umma na binafsi yanashiriki katika mkutano huu.
Vipengele muhimu vya programu vinajumuisha zaidi ya vikao 80 vya majadiliano na takriban warsha 60 za kitaalamu, huku zaidi ya washiriki 2,400 wakitarajiwa kushiriki katika mafunzo hayo.
4315708