IQNA

Maonyesho ya Qur'ani Jamhuri ya Congo

16:23 - July 06, 2014
Habari ID: 1426538
Maonyesho ya kitaifa ya Qur'ani Tukufu yalianza jana katika makao makuu ya Jumuiya ya Kiislamu ya Jamhuri ya Congo kwa mnasaba wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Maonyesho hayo ya Qur'ani ambayo yanafanyika kuadhimisha mwaka 1404 tangu kitabu hicho cha Mwenyezi Mungu kiteremshwe, yalifunguliwa na kiongozi wa Jumuiya ya Kiislamu ya Congo na mabalozi wa nchi za Kiislamu katika ukumbi wa al Kauthar.
Maonyesho hayo pia yana nakala mbalimbali za chapa ya Qur'ani Tukufu kwa lugha tofauti za Kiafrika na baadhi ya zana zinazonasibishwa kwa Mtume Muhammad (saw) kama mavazi yake. Maonyesho hayo yataendelea hadi tarehe 25 Julai.
Baadhi ya watu waliotembelea maonyesho hayo pia wametunukiwa zawadi za tarjumi ya Qur'ani Tukufu. 
1426210

Kishikizo: qur'ani Congo, maonyesho
captcha