Maonyesho haya yanayojulikana kama "Nyumba ya Kwanza", yanawasilishwa katika lugha 10 na yanaeleza historia ya ujenzi wa Kaaba katika vipindi tofauti vya historia, kuanzia wakati wa Nabii Ibrahim (AS) hadi sasa.
Waislamu kote duniani huelekea Kaaba wanaposwali.
Maonyesho haya, yanayofanyika katika sehemu ya upanuzi wa Msikiti Mkuu, yanawapa wageni na mahujaji fursa ya kipekee ya kufuatilia hatua za ujenzi wa Kaaba kupitia maonyesho ya picha, michoro, vitu vya kihistoria, na skrini shirikishi.
Maonyesho haya yameandaliwa na Mamlaka Kuu ya Uangalizi wa Misikiti Miwili Mitukufu wakati wa Ramadhani, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kuwatambulisha Waislamu historia ya Msikiti Mkuu na maeneo yake muhimu kwa kutumia teknolojia za kisasa za mawasiliano.
Mada kuu za maonyesho haya zinajikita katika:
Ramadhani kwa kawaida huwa ni msimu wa kilele wa Umrah, au hija ndogo, katika Msikiti Mkuu, huku mamlaka zikijiandaa kikamilifu kukabiliana na wingi wa waumini.
Msimu wa sasa wa Umrah, ambao unaweza kufanywa mwaka mzima, ulianza mwishoni mwa Juni baada ya kumalizika kwa Hija ya kila mwaka.
3492251