IQNA

9:55 - January 05, 2009
Habari ID: 1727594

Uturuki, mwenyekiti wa kikao cha Jumuiya ya Nchi za Kiislamu

Kikao cha dharura cha Muungano wa Mabunge ya Kiislamu ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Nchi za Kiislamu OIC kitafanyika siku ya Jumatano ijayo huko Istanbul nchini Uturuki kwa lengo la kuchunguza mashambulio ya kinyama yanayofanywa na Wazayuni wa Israel huko katika Ukanda wa Gaza.

Msemaji wa Bunge la Uturuki amewapelekea barua wenzake katika kamati andamizi ya muungano huo wa mabunge akiwafahamisha juu ya mipango ya kufanyika kikao hicho cha dharura.
Kikao hicho ambacho kitahudhuriwa na Spika wa muungano huo kitajadili mashambulio ya utawala haramu wa Israel na mauaji ya umati yanayotekelezwa na utawala huo dhidi ya watu wasio na ulinzi katika Ukanda wa Gaza.
Kamati Andamizi ya Muungano wa Mabungu ya Kiislamu ina wanachama 50 zikiwemo nchi za Uturuki, Nigeria, Misri, Mali, Azerbajan, Iran, Algeria, Saudi Arabia, Chad na Benin. 343555
captcha