IQNA

Haram Tukufu ya Imam Hussein (AS) katika Siku ya Arbaeen

15:48 - August 05, 2026
Habari ID: 3482587
IQNA – Matembezi ya Arbaeen yalifanyika mjini Karbala, ikiwemo katika Haram Tukufu ya Imam Hussein (AS), kwa mahudhurio yenye hamasa kubwa ya wapenzi na wafuasi wa Bwana wa Mashahidi, Imam Hussein (AS) siku ya Jumanne.

Majlisi ya maombolezo ya Arbaeen, ambayo mwaka huu iliangukia tarehe Agosti 4, ni miongoni mwa mikusanyiko mikubwa zaidi ya kidini duniani.

Arbaeen huadhimisha siku ya arobaini baada ya Ashura, kumbukumbu ya kuuawa shahidi kwa mjukuu wa Mtume Muhammad (SAW), Imam Hussein (AS).

Kila mwaka, umati mkubwa wa Waislamu wa Shia humiminika Karbala, ambako iko Haram Tukufu ya Imam Hussein (AS), kwa ajili ya kutekeleza ibada na taratibu za maombolezo.

Mazuwar, hasa kutoka Iraq na Iran, husafiri masafa marefu kwa miguu kuelekea mji huo mtukufu.

Imam Hussein Holy shrine on Day of Arbaeen

Imam Hussein Holy shrine on Day of Arbaeen

Imam Hussein Holy shrine on Day of Arbaeen

 

4367992

captcha