Duru za habari zimeripoti kuwa ujumbe huo wa Kiislamu wa Ulaya unaojumuisha wanasheria na madaktari wa Kiislamu kutoka nchi za bara hilo ulikusudia kuelekea Ukanda wa Gaza kupitia kivuko cha Rafah lakini ulizuiwa na maafisa wa serikali ya Misri.
Shakib bin Makhluf, Mwenyekiti wa Muungano wa Jumuiya za Kiislamu nchini Ufaransa amesema kuwa misaada ya kibinadamu ya ujumbe huo inayojumuisha madawa na zana za kitiba ilivuka mpaka jana na kupelekwa Gaza lakini viongozi wa Misri wameuzuia ujumbe huo kuingia katika eneo hilo.
Shekib Makhluf amesema: Muungano wa Jumuiya za Kiislamu barani Ulaya inalaani vikali jinai za Israel katika Ukanda Gaza na inafanya juhudi kubwa za kusimamisha mauaji ya kizazi ya utawala huo ghasibu dhidi ya wananchi wa eneo hilo. Ameongeza kuwa kwa sasa muungano huo unafanya juhudi za kuwafungulia mashtaka viongozi wa Israel katika mahakama ya kimataifa. 349425