IQNA

Muda wa kujiandikisha kushiriki katika mashindano ya Qur'ani waongezwa

19:00 - February 12, 2009
Habari ID: 1743194
Muda wa kujiandikisha kushiriki katika Olimpiadi ya Nne ya Kimataifa ya Qur'ani na Hadithi iliyoandaliwa na Chuo Kikuu cha Kimataifa cha "Jamiatul Mustafa (SAW) al Alamiya" umeongezwa hadi tarehe 18 Februari.
Ismail Pirnia, mkuu wa Kamati ya Utamaduni ya Olimpiadi ya Nne ya Kimataifa ya Qur'ani na Hadithi ya Chuo Kikuu cha Kimataifa cha "Jamiatul Mustafa (SAW) al Alamiya" kilicho katika mji mtakatifu wa Qum nchini Iran amesema kuwa:"Kwa kuzingaitia idadi kubwa ya waliojiandikisha kushiriki katika duru hii ya Olimpiadi, tumeongeza muda hadi Februari 18 ili kutoa fursa kwa wapendao kushiriki kujiandikisha".
Pirnia ameongeza kuwa muhula wa awali wa kujiandikisha ulikuwa unamalizika tarehe 13 Februari lakini baada ya mashauriano na idara ya maandalizi ya Olimpiadi imeafikiwa kuongeza muhula wa kujiandikisha.
Taasisi za kitaifa na kigeni zilizochini ya Chuo Kikuu cha "Jamiatul Mustafa (SAW) al Alamiya" zinaweza kukubali maombi ya wanaotaka kushiriki hadi tarehe 18 Februari. 362730

captcha