IQNA

11:42 - February 25, 2009
Habari ID: 1748287

Hujuma ya askari usalama wa Saudi Arabia dhidi ya Waislamu wanaozuru Masjidu Nabi (as

Jumatatu alasiri, askari usalama wa Saudi Arabia waliwahujumu Waislamu wa madhehebu ya Shia waliokuwa wamekwenda kuzuru kaburi la Mtume Muhammad (saw) huko katika mji mtakatifu wa Madina na kuwatia nguvuni wengi kati yao.

Kwa mujibu wa televisheni ya Raswid, idadi kubwa ya Waislamu hao ilijeruhiwa na kupelekwa kwa matibabu katika hospitali za az-Zahra, al-Answar na Mfalme Fahd za nchini Saudi Arabia. Ripoti zinasema kuwa, Waislamu hao walikuwa wamekusanyika katika msikiti huo mtakatifu kwa lengo la kufanya maombolezo ya kukumbuka kifo cha mtume Muhammad (saw) na Imam Hassan Mujtaba (as). Wakiwa katika hali hiyo ya mkusayiko, ghafla askari usalama wa Saudia waliwavamia, kuwapiga na kuwatukana, ambapo idadi kadhaa ya Waislamu hao ilijeruhiwa na wengine kutiwa nguvuni. Kati ya watu waliojeruhiwa wamo wanawake na watoto, ambapo hali ya baadhi yao imetangazwa kuwa mbaya sana.
Shambulio hilo la kigaidi la askari usalama wa Saudia dhidi ya Mashia si jipya. Siku chache zilizopita pia yaani siku ya Ijumaa, askari hao waliwashambulia Waislamu wa Kishia waliokuwa wamekwenda kuzuru makaburi ya Baqii ambapo watukufu na viongozi wa Kiislamu wamezikwa, na kuwatawanya na kisha kuwatia nguvuni watano miongoni mwao. 368981
captcha