Washiriki katika zafa hiyo watabeba mabango yenye maandishi ya aya za Qur'ani na hadithi za Mtume (saw) zinazohimiza amani, usawa na uadilifu wa kijamii.
Lengo la harakati hiyo ni kuwaelimisha wananchi wa Zambia sira ya Mtume wa Uislamu.
Zafa hiyo imeidhinishwa rasmi na serikali ya Zambia.
Mkuu wa Kituo cha Utamaduni cha Iran nchini Zambia Sheikh Muhammad Asadi Muwahhid atahutubia zafa hiyo akizungumzia umuhimu wa umoja kati ya Waislamu. 373972