Kipindi hiki ni kipindi cha fahari ya Uislamu na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, na fahari hiyo ni matokeo ya jihadi na kujitolea kwa taifa kubwa la Kiislamu la Iran.
Hayo yamesemwa na Ayatullah Mahmoud Hashimi Shahrudi, Mkuu wa Vyombo vya Mahakama nchini Iran ambaye amewapongeza Waislamu kwa mnasaba wa maadhimisho ya siku ya kuzaliwa Mtume Muhammad (saw) na mjukuu wake Imam Ja'far Swadiq (as).
Amesisitiza juu ya udharura wa kuwepo ushirikiano kati ya viongozi wa vyombo vitatu vya mamlaka kwa ajili ya kukidhi matakwa ya wananchi na kuondoka matatizo yao. 378018