Kikao hicho kitafanyika kwa udhamini wa Chuo cha Fasihi na Elimu ya Ubinadamu na Chuo Kikuu cha Sayyid Muhammad bin Abdallah kwa ushirikiano wa Wizara ya Wakfu na Masuala ya Dini ya Morocco na pia Isesco.
Wanafikra na wasomi kutoka nchi mbalimbali za Kiislamu watashiriki katika kikao hicho na kubadilishana mawazo kuhusiana na historia na maandishi yanayohusiana na maisha ya Mtume Muhammad (Saw) katika mtazamo wa wataalamu wa Marekani wa masuala ya mashariki mwa Dunia na vilevile ya Uislamu.
Washiriki pia watachunguza jinsi shakhsia tukufu ya Mtume Muhammad (saw) inavyoakisiwa katika maandishi ya fasihi na kidini, vyombo vya habari, taasisi za utafiti na vilevile katika mashule ya Marekani. 384812