Kwa mujibu wa shirika la habari la IQNA, lengo la kufanyika mashindano hayo ni kuwafahamisha zaidi wanafunzi mafundisho ya Imam Ali (as), kunyanyua uwezo wa kuhubiri na kushiriki katika kueneza maarifa na mafundisho ya Nahjul Balagha. Mashindano hayo ambayo yamepangwa kufanyika tarehe 31 Mei yamepangwa kufanyika kwa wakati mmoja katika vyuo vinne vya Imam Khomeini, Hujjatiyya, Bintul Huda na Az-Zahra (as). Mashindano hayo yamekaribishwa sana na wanafunzi wa kigeni na hadi sasa wanafunzi 1000 tayari wamesajili majina yao kwa lengo la kushiriki katika mchuano wa kuhifadhi maneno hayo ya hekima ya Imam Ali (as). 405492