IQNA

Kumalizika mashindano ya kusoma Qur'ani Iraq

12:58 - August 24, 2010
Habari ID: 1979991
Mashindano ya saba ya usomaji Qur'ani yalimazika jana Jumatatu katika msikiti wa al-Hashimi katika mji mtakatifu wa Kadhimein nchini Iraq.
Mashindano hayo yaliyoanza tarehe 9 ya mwezi wa Ramadhani yaliandaliwa na Tasisi ya Qur'ani ya al-Iraqiyya katika mji wa Kadhimein na yamemalizika kwa kutuzwa washindi wa mashindano hayo. Mashindano yaliyotajwa yaliwajumuisha wasomaji Qur'ani kutoka mikoa mbalimbali ya Iraq. Mwishoni mwa sherehe za kuhitimisha mashindano hayo, Farajullah Shadhili, refa mashuhuri wa kimataifa wa Qur'ani alimtembelea Rafi' al-Aamiri mkuu wa Taasisi ya Qur'ani ya al-Iraqiyya na wasimamizi kadhaa wa taasisi hiyo na kuwatakia funga njema ya mwezi mtukufu wa Ramadhani pamoja na wananchi wote wa Iraq. Vilevile ameishukuru Taasisi ya Qur'ani ya al-Iraqiyya kutokana na shughuli zake za kuhudumia Qur'ani Tukufu pamoja na kuandaa mashindano ya usomaji wa kitabu hiki kitakatifu. 639937
captcha