IQNA

Utafiti wa Umoja wa Mataifa kuhusu hujuma ya Wazayuni dhidi ya Msafara wa Ghaza

15:14 - August 25, 2010
Habari ID: 1981209
Wakaguzi kutoka Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa wameanza uchunguzi kuhusu hujuma ya jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya msafara wa meli za misaada zilizokuwa zikielekea Ghaza mwezi Mei mwaka huu.
Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA nchini Uturuki, timu ya wakaguzi hao itawahoji raia wa Uturuki walioshuhudia hujuma hiyo ya kinyama iliyotekelezwa na vikosi vya Wazayuni katika maji ya kimataifa.
Itakumbukwa kuwa katika hujuma hiyo ya maharamia wa kiserikali wa utawwala wa Kizayuni wa Israel, wanaharakati tisa wa Uturuki waliuawa shahidi na makumi ya wengine kujeruhiwa. Aidha maharamia hao wa jeshi la wanamaji la utawala haramu wa Israeli walipora mali binafasi za wanaharakati hao wa haki za binadamu waliokuwa wakiwapelekea misaada Wapalestina wanaokabiliwa na mzingiro katika Ukanda wa Ghaza.
640754

captcha