Mkuu wa kitengo cha operesheni za masuala ya tiba na huduma cha Wizara ya Afya ya Iraq Dakta Jasib Latif Ali amewaambia waandishi habari kwamba wizara hiyo inajitayarisha kwa ajili ya shughuli ya maombolezo ya kukumbuka siku ya kuuawa shahidi Imam Ali (as) inayosadifiana na tarehe 21 mwezi wa Ramadhami na imetayarisha vituo makhsusi vya afya katika mikoa ya Najaf, Karbala na mikoa jirani.
Ameongeza kuwa vituo hivyo vya afya vimeboresha kiwango cha huduma za kiafya na kudhamini akiba ya dawa na suhula nyingine za kitiba.
Latif Ali amewataka watu wanaozuru maeneo hayo matakatifu hususan watoto wadogo kujiepusha na vyakula au vinywaji visivyokuwa na kiwango kinachotakikana cha afya kwa ajili ya kulinda afya zao. 644344