IQNA

Ufaransa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Taathira za Dini katika Mienendo ya Kijamii

15:48 - September 12, 2010
Habari ID: 1992021
Mkutano wa Taathira za Dini katika Mienendo ya Kijamii umepangwa kufanyika nchini Ufaransa tarehe 26 Novemba. Mkutano huo utasimamiwa na Jumuiya ya Elimu Nafsi ya Ufaransa.
Jumuiya hiyo imetoa wito kwa wanachuo, watafiti na wataalamu wa masuala ya kijamii na kidini kutuma makala zao kuhusu maudhui hiyo kwa sekretarieti ya mkutano huo hadi kufikia tarehe 10 Oktoba.
Baada ya kuchunguzwa, makala bora zitateulia na waandishi wake wataalikwa kushiriki kwenye mkutano huo nchini Ufaransa.
Waandishi wa makala hizo wanapasa kutambua kwamba makala zao zinapaswa kuzungumzia jamii ambazo si za kidini zilizoathiriwa na dini, kwa mfano taathira za dini ya Kiislamu kwa watu wa Ulaya. 652700
captcha