IQNA

12:24 - September 30, 2010
Habari ID: 2004466

Kanisa la Wisconsin kuwa mwenyeji wa vikao vya "Ujue Uislamu"

Vikao vya Ujue Uislamu vinatazamiwa kufanyika tarehe 12, 19 na 26 Oktoba na tarehe 2 Novemba katika kanisa la St. John Apyskopal kwenye jimbo la Wisconsin nchini Marekani.

Vikao hivyo ambavyo vitafanyika chini ya anwani ya 'Uislamu, dini ya umaridadi, hakika na upendo', vinalenga kuwafundisha wafuasi wa dini myingine mafundisho ya dini ya Kiislamu.
Baadhi ya maudhui za vikao hivyo ni ada na utamaduni tajiri wa Kiislamu, Uislamu katika jamii ya Marekani, wanawake wa Kiislamu, mwezi wa Ramadhani na sura ya Uislamu katika nchi za Magharibi katika miaka ya hivi karibuni.
Vikao hivyo vya Ujue Uislamu vinafanyika kwa hima ya jumuiya ya uchapishaji wa Moore House. 665829
captcha