IQNA

11:07 - October 16, 2010
Habari ID: 2013292

Kurifishwa sura halisi ya Uislamu katika nchi za Magharibi, jukumu muhimu la al-Azhar

Ahmad al-Tayyib Sheikh wa al-Azhar, amesema kuwa kuutetea Uislamu na matukufu yake pamoja na kuuarifisha kwa njia sahihi katika nchi za Magharibi ni ujumbe na jukumu muhimu la taasisi ya kidini ya al-Azhar.

Akizungumza mbele ya wanafunzi wa chuo hicho huko Cairo, Sheikh al-Tayyib amesema kuwa jukumu muhimu la taasisi hiyo katika zama hizi nyeti ni kuwabainishia walimwengu misingi na mafundisho sahihi ya Uislamu yakiwemo ya kuvumiliana pamoja na kupambana na fitina na tuhuma zisizo na msingi zinazotolewa dhidi ya Uislamu.
Amewataka wanafunzi wa al-Azhar kuzingatia maadili ya Kiislamu na kufanya juhudi za kueneza mafundisho sahihi ya Uislamu kwa kutumia mbinu na misimamo ya wastani huku wakivumilia majukumu ya kutetea thamani za Kiislamu. Amewataka pia wadumishe mawasiliano yao na vyuo vikuu kupitia Jumuiya ya Kimataifa ya Wanafunzi wa al-Azhar. 675294
captcha