Kikao hicho kitahudhuriwa na wanasiasa, wataalamu wa masuala ya utamaduni na jamii na viongozi wa kidini wa Kiislamu na Kikristo.
Sabah Mahmoud, mtaalamu wa anthropolojia katika Chuo Kikuu cha California atahutubia kikao hicho akiwasilisha uchunguzi wake wa miaka kadhaa kuhusu uhuru wa dini na utamaduni katika eneo la Mashariki ya Kati na Ulaya.
Vilevile Philipe Natwin ambaye pia ni mtaalamu wa anthropolojia anayefanya uchunguzi kuhusu ibada za Waislamu katika eneo la Goutte d' Or mjini Paris na msikiti wa al Fat'h, atazungumzia uhuru wa kidini wa Waislamu na utekelezaji wa ibada za kila siku katika misikiti ya Paris. 697795