IQNA

Khartoum, mwenyeji wa kongamano la uwekezaji elimu ya watu wazima

12:55 - December 26, 2010
Habari ID: 2053276
Kongamano la uwekezaji katika sekta ya elimu kwa watu wazima limepangwa kufanyika Jumatatu hadi Alkhamisi za tarehe 27 hadi 30 za mwezi huu wa Disemba mjini Khartoum Sudan.
Kongamano hilo linadhaminiwa na Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni la Umoja wa Nchi za Kiislamu ISESCO. Shirika hilo linashirikiana na Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni la Umoja wa Mataifa pamoja na Kamisheni ya Kitaifa ya Elimu, Sayansi na Utamaduni ya Sudan katika kuandaa kongamano hilo.
Zaidi ya wasomi na wanafikra kutoka nchi kadhaa za Kiislamu watashiriki katika kongamano hilo kwa ajili ya kuchunguza njia za kushajiisha uwekezaji katika sekta ya elimu ya watu wazima katika nchi za Kiislamu, wanachama wa Umoja wa Nchi za Kiislamu OIC.
Kuimarishwa nguvu kazi, usimamiaji fedha na mifumo ya kifedha pamoja na kuimarisha mawasiliano ya taasisi zinazohusika na uwekezaji katika sekta iliyotajwa ni baadhi ya mambo yatakayojadiliwa katika kongamano hilo. 717629
captcha