Taarifa ya muungano huo imeitahadharisha serikali ya Libya juu ya kuendelezwa umwagaji damu. Imeutaka utawala wa Libya kumcha Mungu katika kuamiliana na wananchi uliowatawala kwa zaidi ya miongo minne na kuogopa adhamu ya Mwenyezi Mungu. Imesema serikali ya Libya inapaswa kuwapa wananchi haki yao ya kujiamulia hatima yao na kufanya marekebisho ya kimsingi.
Vilevile taarifa ya Muungano wa Kimataifa wa Maulamaa wa Kiislamu imeitahadharisha serikali ya Libya kuhusu utumiaji wa silaha za kisasa dhidi ya wananchi.
Taarifa hiyo pia imewataka wanajeshi wa Libya kuacha kukabiliana na wananchi. Aidha imewahimiza wananchi kusimama kidete katika kudai haki zao. 751816