Mfalme Sheikh Hamad bin Issa Al Khalifa wa Bahrain ameamuru kuachiwa huru wanaharakati waliko jela na kusimamishwa kesi zao.
Kwa upande mwingine mwakilishi wa chama cha al Wifaq cha Mashia waliowengi nchini Bahrain Abdul Jalil Ibrahim ambaye pia ni miongoni mwa wapinzani wa utawala wa nchi hiyo amesema inatazamiwa kuwa wanaharakati 25 wa kambi ya upinzani wataachiwa huru.
Ameongeza kuwa kuachiwa huru wafungwa wa kisiasa ni moja kati ya matakwa ya wapinzani wanaoandamana kwa ajili ya kukubali kufanya mazungumzo na serikali ya Bahrain. 752493