Sheikh al-Mulla amesema katika taarifa yake kwamba tayari uchochezi wa makundi hayo umepelekea kuchomwa moto makaburi ya viongozi wa Kishia katika baadhi ya mikoa ya Misri jambo ambalo limeamsha hasira ya watu wa Misri na kupelekea wanazuoni wa al-Azhar pamoja na Mufti wa Misri kulaani vikali kitendo hicho kisicho cha kiutu. Amewasifu wanaozuoni hao wa Misri kutokana na msimamo wao wa kukemea kuharibiwa na kuchomwa moto makaburi ya mawalii wa Mwenyezi Mungu wa madhehebu ya Shia na kuongeza kuwa lengo la wahusika wa kitendo hicho cha aibu ni kuzusha fitina na mfarakano katika ulimwengu wa Kiislamu. Sheikh al-Mulla amewataka wanazuoni wote wa Kiislamu kuchukua hatua za dharura ili kuzuia kukaririwa kwa vitendo kama hivyo vya uchochezi wa kimadhehebu. 771541