IQNA

13:27 - May 04, 2011
Habari ID: 2117260

HRW yataka kufutiliwa mbali hukumu ya kifo dhidi ya waandamanaji

Shirika la kimataifa la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch lililo na makao makuu yake mjini New York Marekani limeutaka utawala wa kifalme wa Bahrain kufutilia mbali hukumu ya kifo uliotoa dhidi ya waandamanaji wanne wa Kishia nchini humo.

Taarifa ya shirika hilo imesema hukumu iliyotolewa na mahakama ya kijeshi dhidi ya watu hao waliotiwa nguvuni katika maandamano ya kulalamikia ukandamizaji wa utawala huo dhidi ya watu wasio na hatia inapaswa kufutwa mara moja.
Shirika hilo pia limetaka waandamanaji wengine waliotiwa nguvuni na utawala wa Bahrain bila kuruhusiwa kuonana na mawakili wao waachiliwe huru mara moja.
Joe Stork, naibu mkuu wa shirika hilo katika kanda ya Mashriki ya Kati na Afrika Kaskazini amesema kuwa hakuna uwezekano wowote wa mahakama hiyo ya kijeshi kuendesha mashtaka dhidi ya watuhumiwa kwa audilifu na kwa mujibu wa sheria, likiwemo suala la kuwaruhusu wawakilishwe na mawakili wao.
Watu saba waliofikishwa mbele ya mahakama hiyo ya kijeshi ni raia wa kwanza wasiokuwa wanajeshi kuwahi kuhukumiwa katika mahakama hiyo ya kuogofya. 785682
captcha