Kwa mujibu wa gazeti la Imarati la al-Khalij, hicho kitakuwa kikao cha kumi kuandaliwa na chuo kilichotajwa ambapo wasomi na wanafikra kutoka nchi mbalimbali hushiriki na kutoa maoni yake kuhusiana na masuala tofauti ya Kiislamu.
Waandaaji wa kikao hicho wamesema kuwa wamechagua mada ya wakfu kujadiliwa katika kikao cha mwaka huu kutokana na nafasi muhimu ya wakfu katika kunyanyua uchumi wa ulimwengu wa Kiislamu na kuhuisha mfungamano pamoja na udugu wa Kiislamu.
Vyuo 29 kutoka nchi 16 za Kiarabu na Kiislamu na vilevile Marekani pamoja na taasisi kadhaa za utafiti zimealikwa kushiriki katika kikao hicho. 786780