IQNA

Msichana Muirani ashinda Mashindano ya Qur'ani kwa wenye ulemavu wa macho duniani

18:17 - December 08, 2025
Habari ID: 3481630
IQNA – Msichana Muirani ambaye amekamilisha kuhifadhi Qur'ani yote ameshika nafasi ya kwanza katika mashindano ya Qur'an kwa walio na ulemavu wa macho katika ulimwengu wa Kiislamu.

Zahra Khalili Samarin alishinda nafasi ya juu katika Mashindano ya 10 ya Kimataifa ya Qur'ani kwa Wenye Ulemavu wa Macho, yaliyofanyika kutoka Desemba 4 hadi 7 huko Jakarta, mji mkuu wa Indonesia. Khalili Samarin alifikia hatua ya mwisho ya mashindano baada ya kupita hatua ya awali. 

Mashindano haya ya Qur'ani kwa  walio na ulemavu wa macho yalifanyika ili kusaidia vijana wenye vipaji katika uwanja wa Qur'ani miongoni mwa wale walio na ulemavu wa macho, kuboresha nafasi yao katika jamii, na kuendeleza uwezo wao wa kiakili katika fani ya kukumbuka na kusoma Quran Tukufu.

3495652

captcha