IQNA

14:02 - June 02, 2011
Habari ID: 2132731

Malaysia kushirikiana na Misri katika masomo ya mfumo wa kifedha wa Kiislamu

Malasia inalenga kushirikiana na Misri na Saudi Arabi ili kuanzisha vituo vya kielimu vya uchumi wa Kiislamu ili kuinua kiwango cha wasomi wa masuala ya kifedha ya Kiislamu.

Jamil Khir Baharom Waziri katika Ofisi ya Waziri Mkuu amesema amemtaka mkurugenzi wa Mohamad Sheikh Abdul Aziz Baitulmal Professional Institute (IPB) kufuatilia suala hilo ili wanafunzi wa Malaysia wasiende tena katika nchi hizo kwa ajili ya masomo ya masuala ya kiuchumi na kifedha. Amesema Malaysia inataka kuwa na wasomi wenye umahiri katika masuala ya mfumo wa banki na kiuchumi wa Kiislamu.
Jamil Khir amesema serikali pia imetekeleza mipango kadhaa za kuimarisha mfumo wa kifedha wa Kiislamu nchini Malaysia.
802686
captcha