IQNA

Maadhimisho ya kuzaliwa Imam Ali (as) kufanyika katika kituo cha Kiislamu cha Austria

18:28 - June 15, 2011
Habari ID: 2138973
Kituo cha Kiislamu cha Imam Ali (as) katika mji wa Vienna nchini Austria, leo Jumatano kinaandaa sherehe maalumu ya kuadhimisha uzawa wa Imam huyo mtukufu wa Nyumba ya Mtume (saw).
Kwa mujibu wa idara ya uhusiano wa umma ya kituo hicho, maadhimisho hayo ambayo yatahudhuriwa na wapenzi wa Ahlul Beit (as) yamepangwa kuanza saa mbili usiku kwa wakati wa nchi hiyo.
Hujjatul Islam wal Muslimeen Husseini amealikwa kuzungumza katika sherehe hiyo muhimu ya Kiislamu, ambapo atazungumzia shakhsia na matukufu ya Imam Ali (as).
Kituo Cha Kiislamu cha Imam Ali (as) kimewaalika wapenzi na wafuasi wote wa Watu wa Nyumba ya Mtume (saw) kuhudhuria sherehe hiyo. 809280
captcha