Katika salamu zake Ihsanoglu amesema: ‘Natoa salamu zangu za kheri na fanaka kwa Waislamu wote duniani na namuomba Mwenyezi Mungu akubali Saumu, Sala na amali zao njema. Kuwadia mwezi huu mtukufu ni wakati muafaka wa kusisitiza juu ya thamani aali za Kiislamu na umuhimu wa umoja wa Waislamu. Ni jambo la kusikitisha kuwa mwezi wa Ramadhani umewadia wakati maeneo kadhaa ya Waislamu duniani yanakumbwa na vita, masaibu na maafa ya kibinaadamu’.
Katibu Mkuu wa OIC pia ametoa wito kwa Waislamu duniani kuwasaidia Wasomali wanaokumbwa na maafa ya njaa.
835712