Kwa mujibu wa gazeti la Al Khabar la Algeria, Sheikh Qardhawi amesema: “Lakabu ya ‘Mwamko wa Kiislamu’ yaliyopewa matukio ya mapinduzi hayo inatosha na ni nani aliyefikiri matukio haya yatajiri”.
Akizungumza mbele ya hadhara ya vijana, Sheikh Qaradhawi mwenye makao yake huko Doha, Qatar ameongeza kuwa: “Baada ya utawala wa Maliberali na Wasekula, sasa umefika wakati wa wanaharakati wa Kiislamu. Ni muhimu wanaharakati wa Kiislamu watafakari namna ya kuchukua kwa mara nyingine uongozi wa dunia”.
Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Maulamaa Waislamu amesema Misri sasa iko tayari kuanzisha serikali ya Kimataifa ya Kiislamu.
Amesema kinyume na mifumo ya Kiliberali na Kisekula, mfumo wa Kiislamu hautakuwa na hadaa wala ufisadi bali ni wakati wa sayansi, amali njema na bidii.
856762