Catherine Ashton ameliambia Bunge la Ulaya kwamba Israel inapaswa kufuta kibali cha ujenzi wa nyumba 1100 za walowezi wa Kiyahudi katika eneo linalokaliwa kwa mabavu la Baitul Muqaddas Mashariki.
Ashton ameelezea kusikitishwa kwake na kuendelea ujenzi wa vitongoji vya walowezi wa Kizayuni katika ardhi za Palestina na kusisitiza kuwa ujenzi huo unakwamisha mazungumzo ya amani.
Kwa upande wake Marekani imeutaja mpango huo wa Israel wa kuidhinisha ujenzi wa nyumba mpya za walowezi wa Kiyahudi katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu za Israel kuwa inakatisha moyo. 869125